Header Ads


Breaking News
recent

HILI NDIO JAMBO ALILO LIFANYA MKAPA NA KUPELEKEA MWALIMU 

( NYERERE ) AMUITE NYUMBANI KWAKE ( MSASANI ) HARAKA SANA!



Baba  wa  Taifa, Hayati  Mwalimu  Julius  Kambarage  Nyerere.


MKAPA   NA   KUITWA  MSASANI.
“ MWAKA  1965  nilikubali  ombi  la  uongozi  wa    Shirika  la  Utangazaji  la  Tanganyika  ( TBC)  kusoma  taarifa  ya  habari  kwa  lugha  ya  kiingereza.  Siku  moja  baada  ya  kusoma  taarifa  ya  saa  moja  usiku, ilipigwa   simu  chumba  cha  habari, ikiniagiza  niende  mara  moja   Msasani  ( nyumbani  kwa  Mwalimu  )  kwani  Rais  alitaka  kuniona.



Rais  Mstaafu   Mh. Mzee  Benjamin  William  Mkapa.

Moyo  ulidunda  lakini  nilipo wasili  Mwalimu  alinituliza  akaniambia  anataka  nikubali  wadhifa  wa  kuwa   Mhariri  Mtendaji  wa  magazeti  ya  chama  ( TANU )  ya  Nationalist  na  Uhuru “
Maneno  hayo  ni  ya  Rais  wa  Awamu  ya  Tatu, Mzee  Benjamin  William  Mkapa, na  yamo  katika  waraka  wake  wa  Desemba  2011  alioliandikia  gazeti  la  Uhuru  wakati  likisherehekea  miaka  50  tangu  lianzishwe.
Mbali  ya  kuongoza  magazeti  hayo, Mzee Mkapa  alipata  pia  kuwa  Waziri  wa  Habari  na  pia  Waziri  wa  Mambo  ya  Nje.  Ali iongoza  Tanzania  kama  Rais  kuanzia  mwaka  1995  hadi  2005.  Nyerere  alimpigia  kampeni  ya  nguvu  mwaka  1995  ambapo  alipata  ushindi  wa  kishindo.

Inatoka  kwenye  gazeti  la  Raia  Mwema, toleo  Na. 346, Jumatano  Aprili  9, 2 014.

No comments:

Lazaro Masika. Powered by Blogger.